Zamu ya Taj Mall : Ubomoaji wa jumba hilo almaarufu Airgate Mall umeanza

  • 6 years ago
Ubomoaji wa jumba la Airgate mall lilotambulika kama Taj Mall hapo awali uling'oa nanga hii Jumamosi huku shughuli hiyo ikikumbwa na hali ya mshike mshike.

Rabsha zilizotokana na uporaji wa mali kutoka kwa wananchi waliotaka kuiba bidhaa kwenye duka la Rams miongoni mwa maduka ambayo wenyeji walikosa kuhama.

Aidha mmiliki wa Taj Mall Ramesh Chandaria Gorasia ametishia kuelekea kortini kuwashtaki wanaobomoa jumba lake licha ya kupewa ilani ya kuhama mwezi moja uliopita.

Recommended